Tuesday, 21 May 2024

SUZAN KUNAMBI ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU UWT

Wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa chini ya Makamu Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar wakiwa kwenye kikao kilichomchagua Suzani Kunambi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania.
Makamu Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar  Dkt. Hussein Ali Mwinyi  akiwa na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dkt.Emmanuel Nchimbi wakitoka kwenye kikao hicho. 

Saturday, 4 May 2024

CHATANDA ASHIRIKI MAZISHI YA ALIYEKUWA MWENYEKITI UWT SENGEREMA, JANE MSOGA

Mwenyekiti  wa Umoja wa Wanawake Tanzania Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) (kushoto) akiwa kwenye ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti Umoja wa Wanawake Wilaya ya Sengerema Ndg. Jane James Msoga iliyofanyika Mei 3, 2024 katika  Kanisa la AICT (African Inland Church Of Tanzania)

 ..............................

Na Mwandishi Wetu, Mwanza

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) amefika Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza katika Kanisa la AICT (African Inland Church Of Tanzania) kwaajili ya kushiriki Ibada ya Mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti Umoja wa Wanawake Wilaya ya Sengerema Ndg. Jane James Msoga ambaye alifariki  Dunia tarehe 30.04.2024 Katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Seko Toure.  

Mwenyekiti Chatanda akiwa Sengerema amepokelewa na viongozi wa Chama na Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya Bi. Senyi Ngaga na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Wajumbe Kamati ya Siasa Wilaya, Wenyeviti wa UWT Wilaya sita za Mwanza. 

Marehemu Jane ameacha Mume na Watoto 11 wakiwemo watoto wakike 7  na Wakiume 4. Mwili wake unatarajia kuhifadhiwa katika nyumba yake ya Milele Sengerema Mjini Kata ya Nyampurukano Mei 3, 2024. 

Mazishi hayo upande wa Serikali yameongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ndg. Said Mtanda na kuhudhuriwa na Wakuu wa Wilaya Sengerema na Misungwi, Mjumbe Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Viti 20 Tanzania Bara Ndg. Ellen Bogohe, Mwenyekiti CCM Sengerema, viongozi wa UWT Mkoa wa Shinyanga, Wajumbe Baraza Kuu UWT Taifa, Mbunge Jimbo la Buchosa na Sengerema, Wabunge Viti Maalum Mkoa wa Mwanza. 

Mwenyekiti  wa Umoja wa Wanawake Tanzania Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC), akiwafariji wafiwa..
Taswira ya ibada hiyo.
Jeneza lenye mwili wa marehemu likiwa kanisani wakati wa ibada hiyo.
 

Thursday, 25 April 2024

RAIS DKT. MWINYI AKOSHWA NA MDAHALO WA WANAWAKE NA MUUNGANO, AIPONGEZA UWT.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwasilimia Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  walipowasili katika ukumbi wa mkutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kulifungua Kongamano la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)

...........................

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi  ameipongeza Jumuiya  ya  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kazi kubwa waliyoifanya kuwaletea maendeleo wanawake na kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuandaa mdahalo wa wanawake na Muungano.

 Pia, ameupongeza umoja huo kwa kuendelea kuwa kinara katika kubuni na kutengeneza mambo mbalimbali yenye lengo la kuimarisha CCM, kikiunganisha na wananchi na kuimarisha umoja na mshikamano na wananchi.

Dkt. Mwinyi amesema hayo jijini Dar es Salaam leo Aprili 25, 2024 alipofungua mdahalo wa kitaifa wa Wanawake na Muungano uliondaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City.

Mdahalo huo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wake za viongozi  wakuu wastaafu, mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wawakilishi, wananchi na wanachama wa jumuiya hiyo na wa CCM.

Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda amesema wanafanya mdahalo wa kuelekea miaka 60 ya Muungano na kujadili nafasi ya mwanamke katika kipindi cha nyuma,sasa na kijacho

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa UWT, Ndg.Zainab Shomari amesema muungano huo uliletwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar zikiwa huru, haukuwa wa kuchanganya mchanga tu, bali wa kidamu  kwa kuwa Zanzibar kuna watu wa makabila mbalimbali.

Washiriki  wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo.(Picha na Ikulu)

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akiwa na Wake wa Viongozi wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifungua Kongamano hilo lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.(Picha na Ikulu)

WASHIRIKI wa Kongamano na Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishingilia wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan, akipokewa kwa niaba Mhe.Wanu Hafidh Ameir, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi,akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume Mama Fatma Karume,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)  

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhiwa Zawadi Maalum ya Picha iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa mchango wake, akikabidhiwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatanda, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano  kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)   

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,i lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)

VIONGOZI Wastaafu wa UWT wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024 na kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, lililofanyika katika ukumbi wa Mlomani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)

 

Wednesday, 24 April 2024

UWT YAMPONGEZA MKE WA WAZIRI MKUU MSTAAFU MALECELA KWA MALEZI BORA KWA MME WAKE

Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. John Samwel Malecela akizungumza kwenye hafla ya kutimiza miaka 90 tangu azaliwe iliyofanyika Kilimani nyumbani kwake jijini Dodoma Aprili 21, 2024. Kushoto ni mgeni rasmi wa hafla hiyo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia  ni Makamu Mwenyekiti wa CC, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

.................................

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  Mary  Chatanda (MCC) amemshukuru Mungu kwa kumjaalia afya na umri mrefu Waziri Mkuu mstaafu Dkt John Samwel Malecela sambamba na kumpongeza Mama Anne Malecela kwa kuwajibika vyema na kumuhudumia mumewe.

Mwenyekiti Chatanda aliyasema hayo  Aprili 21, 2024 wakati wa hafla ya kumpongeza Dkt. John Samwel Malecela kwa kutimiza miaka 90 ya kuzaliwa kwake ambapo Mgeni rasmi wa hafla hiyo alikuwa Dkt Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar.

Aidha Chatanda , Mary Chatanda , amempongeza Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Anne Kilango Malecela kwa matunzo na malezi mazuri kwa Mume wake Dkt. John Samwel Malecela ambaye ameendelea kuwa na afya na siha njema.

"Tunakupongeza Mama Yetu Anna Kilango Malecela kwa kumtunza vizuri mume wako ambaye amelitumikia Taifa ili kwa uzalendo mkubwa katika ngazi mbalimbali," alisema Chatanda.

Katika hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi kadhaa wa Seriakali na CCM akiwemo Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Abdulrahman Kinana. 

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  Mary  Chatanda akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  Mary  Chatanda, akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Abdulrahman Kinana. 

Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda akionesha furaha yake kwenye hafla hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Abdulrahman Kinana. akizungumza kwenye hafla hiyo.
Hafla ikiendelea.
Hafla ikiendelea.
Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. John Samwel Malecela akisoma kitabu kwenye hafla hiyo.
Wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo.
 

MWENYEKITI UWT TAIFA ALIVYOWAFARIJI WAFIWA , WAATHIRIKA WA MAFURIKO IFAKARA


.......................

Na Dotto Mwaibale

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda akiwa na viongozi wa umoja huo ngazi ya Mkoa wa Morogoro na Wilaya ya Kilombero Aprili 23, 2024 walifanya tendo la huruma kwa kuwapa mkono wa pole kwa wafiwa na waathirika wa mafuriko yaliyo tokea Ifakara mkoani humo.

Akizungumza wakati wa kutoa pole hiyo Chatanda alisema waliona ni vizuri kufika kutoa pole hiyo kufuatia athari kubwa iliyoletwa na mafuriko hayo ikiwa ni pamoja na vifo, wananchi kukosa makazi ya kuishi sambamba na uharibifu wa mali na miundombinu ya barabara.

Mmoja wa waathirika wa mafuriko hayo akizungumzia mafuriko hayo.
Chatanda akikabidhi pole hiyo kwa waathirika
Pole hiyo ikitolewa.
Pole ikitolewa.
Chatanda akizungumza na waathirika hao. 

MDAHALO WA KITAIFA WA WANAWAKE NA MUUNGANO KUFANYIKA KESHO MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan

...............................

Na Dotto Mwaibale

WAKATI tukielekea  Maadhimisho ya siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yatakayofanyika Aprili 26, 2024, Umoja wa Wanawake Tanzania ( UWT ) umeandaa mdahalo wa Kitaifa wenye Dhima ya Nafasi ya Wanawake ndani ya miaka 60 ya Muungano. Tulipotoka, Tulipo na Tunapoelekea litakalofanyika kesho Aprili 25, 2024 Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja huo Mary Chatanda akizungumzia kuhusu mdahalo huo alisema maandalizi yote yapo tayari na kuwa utakuwa na mada mbalimbali zitakazo tolewa na wabobezi wa masuala ya kisiasa nchini ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussen Ali Mwinyi.

Chatanda aliwataja wabobezi hao ambao pia walishika nafasi za juu za uongozi hapa nchini kuwa ni Profesa Palamagamba Kabudi ambaye atatoa mada inayohusu Historia ya Nafasi ya Mwanamke katika Muungano na Balozi Amina Salum Ali ambaye atatoa mada inayoelezea Mwanamke na uongozi, faida za Muungano katika ukuaji wa kijinsia (kisiasa, kiuchumi na kijamii)

Aliwataja watoa mada wengine kuwa ni Mama Anna Abdallah ambaye ataelezea mchango wa UWT katika Muungano, Profesa Ruth Meena ambaye atatoa mada inayozungumzia matarajio ya miaka 60 ya Muungano, Nafasi ya mwanamke katika uongozi, ambapo pia Mama Zakia Meghji na viongozi wengine maarufu na wastaafu watakuwepo.

Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda ambaye ametajwa kuwa ni moto wa kuotea mbali usiozimika na timu yake ndio waliouandaa mdahalo huo anatumia nafasi hiyo kuwaalika wananchi  kwenda kuhudhuria mdahalo huo ambao ni muhimu kwa muktaza wa Taifa letu la Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania na kuwa litaanza Saa 2: 00 asubuhi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussen Ali Mwinyi.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania ( UWT ) Taifa, Mary ChatandaMakamu Mwenyekiti wa UWT Taifa, Zainabu ShomariProfesa Palamagamba Kabudi

Profesa  Ruth Meena.
Balozi Amina Salum Ali.
Mama Anna Abdallah.
Mama Zakia Meghji.



 

Saturday, 20 April 2024

FALSAFA YA 4R YAMPATIA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, SHAHADA NYINGINE YA UDAKTARI

 Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa shahada nyinge ya Udaktari. 

 

*Falsafa ya 4R yampatia Rais Samia shahada nyingine ya udaktari 

*Baada ya India, chuo kingine kikuu kikubwa cha Uturuki chamtunuku Rais Samia shahada ya udaktari 

................................

Na Mwandishi Wetu - Zanzibar 

Huku wakiwa wameshika bango lenye kauli mbiu maarufu ya "Songa na Samia," vijana wanaopiga mbizi kwa sarakasi kwenye eneo la Forodhani la Zanzibar, wametoa video yao mpya kuchambua falsafa ya 4R ya Rais Samia Suluhu Hassan kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Siku chache baada ya vijana hao kutoa video yao hiyo, Rais Samia ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari (Honoris Causa) ya Uchumi na Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki kwenye hafla iliyofanyika chuoni hapo Ankara, Uturuki, leo tarehe 18 Aprili, 2024.

Mwezi Oktoba mwaka jana, Rais Samia alitunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa ya kielimu (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru nchini India. huku akiendelea na ziara yake nchini India.

Hadi sasa, Rais Samia ametunukiwa shahada za heshima takribani 4 kutoka vyuo vikuu vikubwa ndani ya nje ya nchi ndani ya miaka mitatu tu ya Urais wake.

Shahada hizo zinatambua jitihada kubwa inayofanywa na Serikali yake kuleta mabadiliko katika mifumo ya kisiasa, kiuchumi na katika sheria zetu za uchaguzi nchini.

Kwenye uongozi wake, Rais Samia anaamini katika kile kinachojulikana kama 4R – ikiwa ni ufupisho wa maneno manne ya lugha ya Kiingereza; Reconcilation (Maridhiano), Resilience (Ustahamiliivu), Reforms (Mabadiliko) na Rebuidlding (Kujanga Upya).

Hizi ndiyo 4R za Rais Samia ambazo zimeleta mafanikio makubwa kwenye uongozi wake tangu aingie madarakani Machi 19, 2021:

MARIDHIANO 

Kwenye kujenga Tanzania bora,.Rais Samia amesema kuwa anatamani kujenga jamii yenye maridhiano na maelewano. Anatamani kujenga umoja pasipo kujali tofauti zetu za kisiasa, kidini, kikabila na nyingine zote.

Hili litawezekana kwa kujenga jamii inayopata haki sawa mbele ya sheria,  isiyobaguana na inayotoa fursa sawa sawa za kiuchumi kwa wote.

Rais Samia anaamini kuwa maridhiano hayawezi kupatikana penye ubaguzi na pale ambapo kuna wanaokosa fursa na haki zao za kiuchumi na kiraia.

USTAHIMILIVU 

Tanzania haiwezi kusonga mbele kama wananchi na viongozi watakuwa legelege kulinda yaliyo yetu. Wahenga walisema Umoja ni Nguvu na namna pekee ya kupambana na changamoto zote zinazoikumba dunia kwa sasa ni kwetu sisi kufanya hivyo kwa Umoja na Mshikamano.

Huko tuendako tutatikiswa na kuyumbishwa. Iwe kiuchumi, kimazingira, kijamii na kisiasa lakini ni lazima tujenge ustahamivu," Rais Samia alisema.

Hii ni kwa sababu hakuna nchi nyingine zaidi ya hii na hapa ndiyo kwetu. Nilitiwa nguvu sana na namna Watanzania walivyopokea tukio la Royal Tour kwa uzalendo wa kipekee.

MABADILIKO

Kuna msemo mmoja maarufu kwamba kitu pekee cha uhakika kwa mwanadamu ni mabadiliko.

Rais Samia amedhamiria kwamba serikali yake itajitahidi kufanya mabadiliko katika mifumo ya kisiasa, kiuchumi na katika sheria zetu za uchaguzi.

Lengo ni kwamba Tanzania iende na wakati na – kama ilivyokuwa wakati mwingine, tujue mapema ni wakati gani wa kufanya jambo hata kama si watu wanaliunga au hawaliungi mkono kwa wakati husika.

Mabadiliko katika sheria za uchaguzi yataleta ushindani wa haki na kuwapa watu fursa ya kuwachagua wawatakao kuwaongoza. Kwenye uchumi, mabadiliko yatakuwa na lengo la kutoa fursa zaidi kwa watu wengi zaidi kunufaika kiuchumi badala ya wachache.

KUJENGA UPYA 

"Ninafahamu kwamba wananchi hawali maridhiano, ustahamivu wala mabadiliko," Rais Samia alisema.

Kama walivyofanya watangulizi wa Rais Samia, lengo kuu linatakiwa kuwa ukuaji wa uchumi wa Tanzania. Uchumi utakaoongeza ajira kwa vijana wetu na utakaofungua fursa kwa makundi yote ya kijamii yaliyo nchini.

Tayari serikali inaendeleza miradi mikubwa ya miundombinu na mengine kwenye sekta ya madini na nishati. Juhudi zilizofanywa kupitia kampeni ya Royal Tour zina lengo la kuzimua sekta muhimu ya utalii iliyoathiriwa sana na ugonjwa wa Covid 19. Katika kilimo serikali inafanya mabadiliko makubwa ili sekta hiyo muhimu ianze kuwa na mchango inaostahili kwenye uchumi wetu.

"Ninaamini kwamba kwa jitihada zetu za R nne, tutaweza kutimiza malengo ya kuwa na mfumo wa vyama vingi vya siasa. Lengo kuu halikuwa kuwa na vyama vingi vya siasa bali lengo lilikuwa kujenga jamii yenye uzalendo, maridhiano, ustahamivu na yenye uchumi unaokua kwa wote na endelevu," Rais Samia alisema.