RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakiwasilimia Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) walipowasili katika ukumbi wa mkutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kulifungua Kongamano la Wanawake na Muungano lililofanyika leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
...........................
Na Mwandishi Wetu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi
ameipongeza Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa kazi
kubwa waliyoifanya kuwaletea maendeleo wanawake na kukiimarisha Chama Cha
Mapinduzi (CCM) pamoja na kuandaa mdahalo wa wanawake na Muungano.
Pia,
ameupongeza umoja huo kwa kuendelea kuwa kinara katika kubuni na kutengeneza
mambo mbalimbali yenye lengo la kuimarisha CCM, kikiunganisha na wananchi na
kuimarisha umoja na mshikamano na wananchi.
Dkt. Mwinyi amesema hayo jijini Dar es Salaam leo
Aprili 25, 2024 alipofungua mdahalo wa kitaifa wa Wanawake na Muungano
uliondaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kufanyika katika ukumbi wa
Mlimani City.
Mdahalo huo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali
wakiwemo wake za viongozi wakuu
wastaafu, mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wawakilishi, wananchi na wanachama
wa jumuiya hiyo na wa CCM.
Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary
Pius Chatanda amesema wanafanya mdahalo wa kuelekea miaka 60 ya Muungano na
kujadili nafasi ya mwanamke katika kipindi cha nyuma,sasa na kijacho
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa UWT,
Ndg.Zainab Shomari amesema muungano huo uliletwa na nchi mbili za Tanganyika na
Zanzibar zikiwa huru, haukuwa wa kuchanganya mchanga tu, bali wa kidamu kwa kuwa Zanzibar kuna watu wa makabila
mbalimbali.
Washiriki wa Kongamano la Wanawake na Muungano
kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika leo
25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akihutubia na kulifungua Kongamano hilo.(Picha na Ikulu)
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akiwa
na Wake wa Viongozi wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Kongamano la Wanawake na
Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akifungua Kongamano hilo lililofanyika leo 25-4-2024 katika ukumbi wa Mlimani
City Jijini Dar es Salaam.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Kongamano na Wanawake na Muungano
kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishingilia wakati
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akihutubia na kulifungua Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani
City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha
iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano
wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan, akipokewa kwa niaba Mhe.Wanu Hafidh
Ameir, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano
lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo
25-4-2024.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi,akimkabidhi Zawadi Maalum ya Picha
iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mjane wa Rais wa Kwanza wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume
Mama Fatma Karume,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na
Muungano lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha
na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akimkabidhiwa Zawadi Maalum ya Picha
iliyotolewa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa mchango wake, akikabidhiwa
na Mwenyekiti wa UWT Taifa Mary Chatanda, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la
Kitaifa la Wanawake na Muungano
kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika
katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na
Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la
Kitaifa la Wanawake na Muungano kuadhimisha Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania,i lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam leo
25-4-2024.(Picha na Ikulu)
VIONGOZI Wastaafu wa UWT wakifuatilia hutuba ya
ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Wanawake na Muungano lililofanyika leo
25-4-2024 na kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, lililofanyika katika ukumbi wa Mlomani
City Jijini Dar es Salaam leo 25-4-2024.(Picha na Ikulu)







No comments:
Post a Comment