Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan
...............................
Na Dotto Mwaibale
WAKATI tukielekea Maadhimisho ya
siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yatakayofanyika Aprili 26, 2024,
Umoja wa Wanawake Tanzania ( UWT ) umeandaa mdahalo wa Kitaifa wenye Dhima ya
Nafasi ya Wanawake ndani ya miaka 60 ya Muungano. Tulipotoka, Tulipo na
Tunapoelekea litakalofanyika kesho Aprili 25, 2024 Ukumbi wa Mlimani City
Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja huo Mary Chatanda akizungumzia kuhusu mdahalo
huo alisema maandalizi yote yapo tayari na kuwa utakuwa na mada mbalimbali
zitakazo tolewa na wabobezi wa masuala ya kisiasa nchini ambapo mgeni rasmi
atakuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussen Ali
Mwinyi.
Chatanda aliwataja wabobezi hao ambao pia walishika nafasi za juu za
uongozi hapa nchini kuwa ni Profesa Palamagamba Kabudi ambaye atatoa mada
inayohusu Historia ya Nafasi ya Mwanamke katika Muungano na Balozi Amina Salum
Ali ambaye atatoa mada inayoelezea Mwanamke na uongozi, faida za Muungano
katika ukuaji wa kijinsia (kisiasa, kiuchumi na kijamii)
Aliwataja watoa mada wengine kuwa ni Mama Anna Abdallah ambaye ataelezea
mchango wa UWT katika Muungano, Profesa Ruth Meena ambaye atatoa mada
inayozungumzia matarajio ya miaka 60 ya Muungano, Nafasi ya mwanamke katika
uongozi, ambapo pia Mama Zakia Meghji na viongozi wengine maarufu na wastaafu
watakuwepo.
Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda ambaye ametajwa kuwa ni moto wa kuotea mbali usiozimika na timu yake ndio waliouandaa mdahalo huo anatumia nafasi hiyo kuwaalika wananchi kwenda kuhudhuria mdahalo huo ambao ni muhimu kwa muktaza wa Taifa letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwa litaanza Saa 2: 00 asubuhi.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania ( UWT ) Taifa, Mary Chatanda
Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa, Zainabu Shomari
Profesa Palamagamba Kabudi
.jpeg)
.jpeg)



No comments:
Post a Comment